- 1,193 viewsDuration: 2:13Vurugu lilishuhudiwa katika kichinjio cha nyama mjini Nanyuki baada ya wadau kudai kuwa kulikuwa na mpango wa kuikodisha kwa wawekezaji binafsi. Wafanyabiashara wa nyama, ambao walikuwa wamesitisha shughuli za uchinjaji kwa sehemu kubwa ya siku na hivyo kupuuza shughuli katika kituo hicho, walidai kuwa serikali ya kaunti ilikuwa inapanga kukodisha kichinjio bila kuwahusisha, hatua ambayo walisema ingeathiri shughuli zao za biashara. Wakizungumza baada ya kikao na serikali ya kaunti, wafanyabiashara hao pia waliikosoa serikali ya kaunti, wakiishutumu kwa kushindwa kuwekeza mapato yanayokusanywa ili kuboresha na kuitunza.