Shughuli za usafiri mjini busia zimekwama huku abiria na wafanyabiashara wakisalia kuhangaika kufuatia mgomo wa kulalamikia ongezeko la bei ya mafuta.
Kulingana na baadhi ya abiria na wafanyabiashara, shughuli zao zilitatizika pakubwa kuanzia mapema hii leo kutokana na mgomo huo, hali ambayo inawapa hofu ya kukadiria hasara maradufu iwapo hali hiyo haitabidilika.. Aidha, baadhi ya madereva wanasema kuwa ni kinaya kubwa kwa bei ya mafuta kupanda hapa nchini ikilinganishwa na taifa jirani la uganda na ilhali mafuta yote yanapitia humu nchini kuelekea mataifa mengine.