- 286 viewsDuration: 3:24Wito unatolewa kwa serikali ya kitaifa kupitia wizara ya mipango maalum kusambaza chakula kwa wakazi wa kaunti ya Taita Taveta kufuatia baa la njaa. Wakazi wa Bughuta eneo bunge la Voi wakisema kukosekana kwa mvua ya kutosha kumesababisha uhaba huo wa chakula huku uhaba wa maji pia ukiwakumba kwa sasa. Wakaazi walioathirika wanasema tatizo la wanyamapori hasa ndovu kushambulia mimea yao pia limechangia uhaba huo wa chakula.