- 669 viewsDuration: 2:42Kizaazaa kilishuhudiwa katika kijiji cha Ciagiini, Mwea, Kaunti ya Kirinyaga baada ya wakazi wenye hasira kuzuia mazishi ya kijana aliyedaiwa kuuawa na mhubiri. Wakazi hao waliandamana na mwili wa marehemu Martin Kara hadi katika Kituo cha Polisi cha Ciagiini wakitaka haki itendeke kuhusiana na kifo chake. Aidha, wakazi hao waliapa kutomzika marehemu hadi haki ipatikane, huku wakiwalaumu maafisa wa polisi kwa madai ya uzembe katika kushughulikia tukio hilo.