- 221 viewsDuration: 2:38Kizaazaa kimeshuhudiwa kijijini Kadawa, eneo la Murinduko, Kaunti ya Kirinyaga, baada ya wakazi wa eneo hilo kuwalazimisha wabunge wawili kutoka kaunti hiyo kuyafungua madarasa matano ya Shule ya Msingi ya Kadawa. Wakazi hao walilalamikia kuchelewa kuzinduliwa kwa ufunguzi wa madarasa hayo miezi miwili baada ya ujenzi kukamilika. Wakazi walisitisha kikao hicho kilichokuwa kikihudhuriwa na Mwakilishi wa Kike Njeri Maina na Seneta Kamau Murango.