Wakenya watakiwa kuzingatia kanuni za trafiki

  • | Citizen TV
    279 views

    Wakenya wametakiwa kuzingatia kanuni za trafiki ili kuepuka maafa barabarani. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kanuni za usalama wa barabarani, afisa wa uchunguzi katika kampuni ya Directline Wilson Maina alibaini kuwa idadi kubwa ya ajali zinasababishwa na kutofuata kanuni za trafiki. Maina aidha aliipongeza serikali kwa kuzindua matumizi ya teknlojia ili kuimarisha usalama wa madereva na abiria. Kulingana na takwimu kutoa mamlaka ya NTSA, zaidi ya watu 1000 wameangamia kutokana na ajali za barabarani kati ya mwezi Januari na Aprili mwaka huu .