- 324 viewsDuration: 4:01Wakulima katika kijiji cha Ruvutiri, eneo la Embu Kaskazini, wanaitaka serikali kuingilia kati kutafuta suluhu kwa dharura kufuatia kuzuka kwa ugonjwa usiojulikana unaoshambulia miti ya makadamia. Wakulima hao wanasema wanapata hasara kubwa huku ugonjwa huo ukiendelea kuenea mashambani na kuhatarisha maisha yao, na sasa wanaitaka serikali kuwatuma wataalamu wa kilimo kubaini chanzo cha ugonjwa huo na kupendekeza njia za kuudhibiti.