- 155 viewsDuration: 1:27Wakulima zaidi ya elfu 22 katika kaunti ya Bungoma wamepokea pembejeo bila malipo kutoka kwa serikali ya kaunti ya bungoma ili kuwasaidia kuzalisha chakula cha kutosha msimu huu wa upanzi. Gavana wa kaunti ya Bungoma Ken Lusaka ambaye aliongoza haflaya ugavi wa pembejeo eneo la namwacha, amesema kuwa wakulima 500 katika wadi zote 45 za kaunti ya Bungoma watanufaika na mpango huo huku serikali ya kaunti ikilenga wale wenye mapato ya chini. Aidha naibu gavana wa kaunti hiyo Jenniffer Mbatiany amesema utoaji wa mbegu na mbolea hizo utasaidia kaunti hiyo kuwa na chakula cha kutosha.