Skip to main content
Skip to main content

Walimu wa sekondari msingi wataka uhuru wa kujisimamia

  • | Citizen TV
    448 views
    Duration: 2:13
    Walimu wa shule za sekondari msingi (JSS) katika Kaunti ya Kwale wameendelea kushinikiza serikali kuwapa uhuru kamili wa kujisimamia badala ya kuendelea kuwa chini ya shule za msingi. Viongozi wa vyama vya walimu vya KUPPET na KEJUSTA wameibua masuala yanayoathiri shule hizo, yakiwemo ukosefu wa uhuru wa kiutawala, miundombinu duni, ukosefu wa mwongozo wazi wa kupandishwa vyeo kwa walimu na kuendelea kwa kandarasi ya muda ya maelfu ya walimu wanagenzi .