- 13,676 viewsDuration: 3:08Wanafunzi tisa wanaodaiwa kusababisha vifo vya wanafunzi wenzao kumi na sita kwenye mkasa wa moto katika shule ya upili ya wasichana ya Utumishi Academy, Gilgil, watasalia seli hadi kesho ambapo mahakama itatoa uamuzi kuhusu iwapo wataachiliwa kwa dhamana au la. Upande wa mashtaka umeiomba mahakama kuruhusu wanafunzi hao wazuiliwe kwa siku thelathini ili uchunguzi ukamilishwe. Maafisa wa usalama waliweka doria kali nje na ndani ya mahakama ya Naivasha wakati washukiwa walipowasilishwa mahakamani.