Wanasheria wapinga mpango wa kuweka hazina za CDF na NGAAF kwenye katiba

  • | Citizen TV
    598 views

    Upinzani umeonekana kutokota kuhusiana na mchakato wa kuziweka hazina za wabunge za CDF na NGAAF pamoja na ile inayosimamiwa na seneti kwenye katiba kupitia mabunge hayo. Baadhi ya mawakili sasa wanasema ni kinyume cha sheria wakisema ni lazima wakenya wahusishwe kupitia kura ya maamuzi. Mawakili hao waliowasilisha hoja katika bunge la kitaifa na lile la seneti wameshikilia kuwa jukumu la wabunge ni kutunga sheria na kufuatilia utekelezaji wake