Wanawake Zimbabwe wajenga makazi kwa ajili ya akina mama wajawazito

  • | VOA Swahili
    29 views
    Wanawake wa Zimbabwe wanawasimamia wanawake wenzao wajawazito wanaoishi vijijini. Kundi la wanawake limekusanya rasilimali ili kujenga makazi kwa ajili ya kina mama wajawazito ambao wanaishi mbali na kliniki. Kwa hakika inaweza kuokoa maisha ya wajawazito ambao hawawezi kufika kwenye kliniki kwa muda muafaka ili kujifungua. #VOASwahili Sauti ya Amerika - Idhaa ya Kiswahili inawafikia zaidi ya watu milioni 100 wanaotembelea tovuti, mitandao ya kijamii, radio na televisheni zetu. Tunawasilisha maudhui kuhusu Afrika Mashariki na Kati kwa nchi takriban 11 huko Afrika na wale walioko ughaibuni na kwingineko duniani. Vipindi vyetu vimejikita katika maudhui mbalimbali ikiwemo habari, vijana, wanawake, siasa, sayansi, teknolojia, afya, biashara, michezo, muziki na burudani na pia tunawashirikisha wasikilizaji wetu.