- 142 viewsWaziri wa Kawi Opiyo Wandayi amesema kuwa kuna mafuta ya kutosha nchini huku akibainisha kuwa meli kadhaa za kusafirisha mafuta ya petroli tayari zimetia nanga katika Bandari ya Mombasa. Akizungumza na wanahabari jijini Nairobi, Wandayi amesema hali ya soko la kimataifa inaashiria kuwa huenda bei ya mafuta ikaanza kushuka katika siku zijazo.