- 945 viewsWaziri wa Kawi Opiyo Wandayi amewataka Wakenya kudumisha amani wakati huu ambao taifa linashuhudia maandamano kuhusu gharama ya maisha na bei ya mafuta. Akizungumza Katika kaunti ya Wajir, Wandayi alisema serikali inaendelea kushughulikia changamoto za bei ya mafuta huku akisisitiza kuwa maandamano yanapaswa kufanyika kwa njia ya amani bila kuhatarisha usalama wa wananchi au kuharibu mali.