Waokoaji: 'Jeshi la Israeli laacha miili mingi mjini Gaza City'
Waokoaji walisema majeshi ya Israeli yameacha darzeni za miili walipoondoka maeneo mbalimbali ya Gaza City usiku baada ya mashambulizi makali yaliyodumu kwa wiki nzima ambayo yalikabiliwa na wapiganaji wa Hamas wakikabiliana nao. Waokoaji walisema wameikusanya kiasi ya miili 60 hadi sasa.,
Jeshi hilo lilitoa kanda ya video Jumatano (Julai 10) ikionyesha kile walichosema ni majeshi ya ardhini yakifanya operesheni Gaza wakati mashauriano ya kusitisha mapigano katika vita vilivyodumu kwa miezi tisa yamepangwa kuanza tena.
Jeshi la Israeli lilisema katika taarifa yake kuwa majeshi yake yalikuwa yanaendelea na operesheni huko Gaza City dhidi ya wanamgambo wa Hamas na washirika wao Islamic Jihad, ambao walisema walikuwa wanafanya mashambulizi kutoka katika kituo cha UNRWA, wakikitumia kama ni ngome yao ya kufanya mashambulizi.
Kulingana na jeshi la Israeli walikuwa wamefanyia operesheni zao katikati mwa Gaza na Shejaiya.
Shirika la habari la Reuters halikuweza kuthibitisha eneo linaloonyeshwa katika kanda ya video. Reuters imeshindwa kupata uthibitisho huru wa tarehe ambayo video hiyo ilichukuliwa.
Vita hiyo ilianza Oktoba 7 wakati wapiganaji kutoka Palestina wa kikundi cha wanamgambo wa Hamas walipovamia mpakani na kushambulia jamii mbalimbali huko Israel, ikiuwa watu 1,200 na kuwateka watu 250, kulingana na idadi iliyotolewa na Israeli.
Shambulizi la Israeli huko Gaza kulipiza kisasi lilianza siku hiyo hiyo kwa kushambulia kwa mabomu na limeendelea kwa miezi tisa pamoja na uvamizi wa ardhini ambapo mamlaka za afya Palestina zinasema imeuwa zaidi ya watu 38,000 na kujeruhi zaidi ya watu 80,000.
Idadi kubwa ya waliojeruhiwa kutokana na vita hivyo imeongeza magonjwa kusambaa na utapiamlo kati ya wakazi asilimia 90 wa Gaza ambapo Umoja wa Mataifa unasema wamekoseshwa makazi, na kuweka shinikizo kubwa kwa mifumo ya afya katika eneo hilo finyu. - Reuters
#Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #mauaji #jeshi #israel #voa #voaswahili #mwandishi #aljazeera #maghazi #wahouthi #marekani #uingereza #shambulizi #dhamar #yemen #hospitali #nasserhospital
26 Apr 2025
- The governor applauded Ruto few days after he signed the multibillion-shillings China deals.
26 Apr 2025
- The Chief Justice can not seem to catch a break as she faces challenges left, right and centre as the head of the Judiciary.
26 Apr 2025
- Through a representative, they said that for some time, their rights have been violated.
26 Apr 2025
- In front of hundreds of world leaders attending the funeral of Pope Francis on Saturday, Italian Cardinal Giovanni Battista Re called for care for migrants, an end to wars, and action on global climate change - Francis' favourite political themes.
26 Apr 2025
- Pope Francis' wooden coffin was carried into St. Peter's Square on Saturday at the start of a funeral Mass attended by a multitude of mourners, including powerful world leaders, clerics and pilgrims.
26 Apr 2025
- Gaza's civil defence agency said Israeli strikes on Saturday killed at least 17 people across the territory, while more were trapped under the rubble after a family home was hit.
26 Apr 2025
- Donald Trump and Volodymyr Zelensky met briefly at Pope Francis's funeral on Saturday, Kyiv said, marking their first encounter since a disastrous White House clash as the US president pushes the Ukrainian to make a peace deal with Russia.
26 Apr 2025
- The governor applauded Ruto few days after he signed the multibillion-shillings China deals.
26 Apr 2025
- While the funeral is the focus, considerable attention is focused on potential diplomatic moves on sidelines.
26 Apr 2025
- Orange Democratic Movement (ODM) leader Raila Odinga has defended the partys decision to work with the government
26 Apr 2025
- The Chief Justice can not seem to catch a break as she faces challenges left, right and centre as the head of the Judiciary.
26 Apr 2025
- Ukrainian President Volodymyr Zelensky and US President Donald Trump have met in Rome ahead of Pope Francis’ funeral. Officials from both parties confirmed the meeting had taken place, with the White House describing it as “very productive”. No further…
26 Apr 2025
- Kisumu County Governor Anyang’ Nyong’o has welcomed President William Ruto’s intention to extend the Standard-Gauge Railway (SGR) to Kisumu. In a statement on Saturday, April 26, 2025, Nyong’o, a perceived critic of the broad-based government, indicated…