- 125 viewsMajeshi ya Israeli Jumanne yameongeza operesheni zake huko Gaza City licha ya maonyo kutoka kwa viongozi wa Hamas kuwa mashambulizi yanaweza kuathiri mazungumzo yanayoendelea ya sitisho la mapigano. Jeshi la Israeli limesema kuwa wanajeshi wake walikuwa wanapiga katika eneo la Shejaiya na limeuwa darzeni ya wanamgambo. Ofisi ya Haki za Binadamu ya UN imeelezea wasiwasi wake Jumanne kuhusu operesheni hiyo na amri za hivi karibuni za Israel zimewataka raia waondoke. Shirika la UN lilisema amri hizo zilizotolewa Jumapili ziliwataka raia kuondoka kuelekea magharibi mwa Gaza City kwa usalama wao, na baadaye kushuhudia Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) limeongeza mashambulizi yake huko. “Ofisi ya Haki za Binadamu ya UN imerejea kueleza wasiwasi wake kuwa amri ya IDF ikiwataka watu kuhama inakanganya, mara kwa mara ikiwaamirisha watu kuondoka kwenda maeneo mengine ambapo operesheni za kijeshi za IDF zinafanyika. Tunarejea wito wetu kwa Israel kufanya juhudi zote kuhakikisha usalama wa raia huko Gaza,” shirika hilo lilisema katika taarifa yake. Wapatanishi nchini Misri wanajaribu kufanikisha kile kinachotafutwa kwa muda mrefu kusitisha mapigano huko Gaza. White House ilisema Jumatatu kuwa maafisa wa Marekani wako Misri kwa majadiliano yanayolenga kupatika kwa makubaliano ya sitisho la mapigano kati ya Israel na Hamas. Wanamgambo wa Palestina waliwauwa takriban watu 1,200 katika shambulizi la kushtukiza na kuwachukua mateka wengine 250 mnamo Oktoba 7, 2023. Shambulizi la kulipiza kisasi la Israel liliofuatia limeuwa zaidi ya Wapalestina 38,000, kulingana na Wizara ya Afya katika eneo hilo, hesabu yao haitofautishi kati ya wapiganaji na raia. - AP, AFP, Reuters #Rafah #Netanyahu #Misri #Hamas #Gaza #Palestina #IDF #GalMeirEizenkot #mauaji #jeshi #israel #voa #voaswahili #mwandishi #aljazeera #maghazi #wahouthi #marekani #uingereza #shambulizi #dhamar #yemen
Wapalestina
- - Kenya-Finland Ties ››
- 14 May 2025 - Safaricom CEO Peter Ndegwa has addressed concerns about the company's involvement in the Social Health Authority (SHA) system, clarifying that its role is limited to the digitisation of the process.
- 14 May 2025 - Sean "Diddy" Combs' former girlfriend, Casandra Ventura, the star prosecution witness at the hip-hop mogul's sex trafficking trial, testified on Tuesday that her music career began to suffer as she increasingly spent her time participating in days of…
- 14 May 2025 - South Africa's unemployment rate rose in the first quarter of this year, with statisticians fretting that increasing numbers of people appear to have given up looking for work.
- 14 May 2025 - Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu said the military will enter Gaza "with full force" in the coming days, despite ongoing ceasefire efforts and the release of a US-Israeli hostage from the war-ravaged territory.
- 14 May 2025 - Finland President Alexander Stubb has hailed the historical Kenyan Gen Z movement witnessed in June last year during the anti-government protests, saying it was a momentous display of democracy.
- 14 May 2025 - Opposition leaders are now claiming that the Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC) nominees presented to Parliament for approval to take up management of the electoral body are a project to rig the 2027 General Election.
- 14 May 2025 - The crisis in the country's education sector continues to deepen, with the latest development being a Ksh.62 billion budget shortfall.
- 14 May 2025 - Tanzanian authorities arrested a senior opposition official as he was departing for a political conference in Belgium, his party said on Tuesday, as fears grow of an escalating crackdown ahead of an October election.
- 14 May 2025 - “No clean water. No toilets. No electricity. No well-planned living environment.” That is how Pastor Evans Moseti describes the one-room mabati house he has called home for the past nine years, its blue iron-sheet walls barely holding back Nairobi’s…
- 14 May 2025 - Eyes on Gachagua and fresh outfit amid moves to entice Mt Kenya