Skip to main content
Skip to main content

Watoto wazidi kusimulia changamoto za karo huku mjadala wa mpito wa elimu ukiendelea

  • | Citizen TV
    349 views
    Duration: 3:33
    Watoto zaidi wamejitokeza kusimulia masaibu yao ya kulazimika kuwacha shule kwa kukosa karo, licha ya serikali kuwaagiza kuripoti shule bila karo wala sare. Baadhi ya watoto hawa wamelazimika kuwacha shule huku wengine wakisema bado wanangoja kujiunga na Gredi ya 10, wakati wenzao wakiendelea na muhula wa pili. Simulizi hizi zinajitokeza huku Wizara ya Elimu ikikana takwimu za Baraza la Mtihani kwamba wanafunzi zaidi ya laki moja na nusu hawakuendelea na masomo ya mpito wa CBE.