Watu 4 waaga dunia Nairobi na wawili Machakos kufuatia mafuriko

  • | KBC Video
    68 views

    Watu wanne wamefariki kufuatia mafuriko katika kaunti ya Nairobi. Kulingana na gavana wa kaunti hiyo Johnson Sakaja, juhudi za kuwatafuta watu wengine sita walioripotiwa kutoweka zinaendelea. Katika kaunti ya Machakos, watu wawili wameaga dunia kufuatia mafuriko katika mtaa wa mabanda wa Kwa Mang'eli huko Athi River. Mafuriko hayo yaliyotokana na mvua kubwa iliyonyesha jana usiku, yalisababisha uharibifu mkubwa katika maeneo kadhaa ya nchi hii huku barabara kadhaa zikiwa hazipitiki. Idara ya utabiri wa hali ya hewa hapa nchini imeonya kuwa mvua kubwa inatarajiwa kuendelea katika maeneo mbali mbali ya nchi hii.

    Connect with KBC Online; Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKN Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1 Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV Check our website: https://www.kbc.co.ke/

    #kbcchannel1 #news #kbclive