- 8,985 viewsDuration: 2:58Watu kadhaa wamejeruhiwa baada ya makundi mawili ya wahuni kukabiliana katika kaunti ya Kisumu. Kwenye kizaazaa hicho, pikipiki zaidi ya tano zikiteketezwa. Ghasia hizo zilitokea baada ya kundi moja kujaribu kuvamia kanisa la ACK St. Stephens, ambako Gavana wa Siaya James Orengo na Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna walikuwa wakihudhuria ibada. Na kama anavyoarifu Laura Otieno, viongozi hao wamekashifu vikali ghasia hizo na kuilaumu serikali kwa kukosa kudhibiti ujambazi wa kisiasa nchini.