- 391 viewsDuration: 2:07Waziri wa Kilimo Mutahi Kagwe amezitaka serikali za kaunti kukumbatia mfumo wa kushirikisha wawekezaji kama njia mojawapo ya kukuza kilimo nchini. Akizungumza kwenye kongamano la kilimo lililoandaliwa na Jumuiya ya kaunti za Pwani mjini Malindi, Kagwe anasema serikali ya kitaifa haiwezi kufadhili sekta hiyo asilimia mia moja. Kadhalika, Kagwe ameonya kuwa endapo ugawaji wa vipande vya ardhi hautadhibitiwa huenda ukaadhiri Kwa sekta ya kilimo nchini.