- 285 viewsDuration: 1:56Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba murkomen amesisitiza kwamba serikali haitalegeza kamba kwenye vita dhidi ya pombe haramu nchini. Wito huu ukiungwa mkono na viongozi wa eneo la mlima kenya wakilalamikia athari ya pombe hiyo mingoni mwa vijana. Akizungumza huko Nyeri Murkomen vile vile amewapa maafisa wa usalama jukumu la kushirikiana na idara zingine za serikali ili kufanikisha vita hivyo. Aidha Murkomen ametoa onyo kali kwa maafisa wa usalama ambao hushirikiama na wafanyi biashara wanaotengeneza na kuuza pombe hiyo, akisema kuwa wataadhibiwa kisheria.