- 5,819 viewsDuration: 50sWaziri wa elimu Julius Migos Ogamba anakutana na viongozi wa vyama vya , IPUCCF, UASU, KUSU na KUDHEIHA kuhusu mgomo unaoendelea wa wahadhiri na wafanyakazi wengine wa vyuo vikuu. Wakiwa kwenye kamati ya bunge hapo jana, Viongozi wa UASU walilegeza msimamo wao wa kutaka kulipwa shilingi bilioni 7.9 kwa mpigo, na kuitisha asilimia 80 katika awamu ya kwanza kisha asilimia 20 walipwe mwakani. hata hivyo, serikali ilishikilia kwamba ingeweza tu kuwalipa kwa awamu mbili za asilimia 50.