- 4,510 viewsDuration: 2:52Wajumbe wa chama cha ODM kaunti ya Nairobi sasa wamemuidhinisha mbunge wa EALA na mwanawe marehemu Raila Odinga Winnie Odinga kuwa mmoja wa manaibu wa chama hicho katika kongamano kuu la chama cha ODM wiki ijayo. Wakiongozwa na mbunge wa Makadara George Aladwa, wanasiasa hao wanasema watawasilisha ombi hilo mbele ya kongamano wakidai kuwa baada ya kifo cha Raila Odinga eneo la Nairobi halina mwakilishi katika uongozi mkuu wa chama .