- 42 viewsZaidi ya wakulima 200 kutoka Kipini Mashariki, kaunti ya Tana River wamepokea miche laki tano ya minazi ili kuendeleza kilimo hicho ambacho kulikuwa kimeanza kudidimia. Wizara ya kilimo ya kaunti hiyo inalenga kuimarisha na uboresha kilimo hicho kwa kuongeza thamani kwa bidhaa zinazokuzwa kaunti ya Kilifi ili kuongeza mapato na kufufua uchumi wa wakulima.Aidha wizara hiyo pia inashirikiana na taasisi za kilimo nchini kwa kuwapa wakulima miche iliyofanyiwa utafiti ili kuongeza uzalishaji .