Mahakama ya kushughulikia kesi za ugaidi iliyo kwenye mahakama ya Kahawa katika Kaunti ya Kiambu inatarajiwa kutoa uamuzi kuhusu iwapo makachero kutoka kitengo cha polisi cha kukabiliana na ugaidi wanapaswa kuruhusiwa kumzuilia mkimbizi wa Uturuki kwa siku 15 ili kukamilisha uchunguzi, au kumwachilia kwa dhamana. Uamuzi huo unajiri kufuatia kukamatwa kwa Ahmet Mustafa Gungor , ambaye alinaswa katika kituo cha Reli ya kisasa jijini Nairobi alipokuwa akisafiri kutoka Mombasa.Ahmet Mustafa alikamatwa kwa tuhuma za kuhusika katika makosa yanayohusiana na ugaidi.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive