- 61,769 viewsDuration: 46sPolisi nchini Afrika Kusini wamemkamata mtoto wa mwisho wa rais wa zamani wa Zimbabwe, Hayati Robert Mugabe, ambaye anakabiliwa na shtaka la jaribio la mauaji kufuatia tukio la kurushiana risasi linalodaiwa kutokea katika nyumba moja huko Johannesburg. Bellarmine Mugabe, 28, alikamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi baada ya mwanaume mwenye umri wa miaka 23 kupigwa risasi na kujeruhiwa. #bbcswahili #afrikakusini #Zimbabwe Subscribe kupata video motomoto kila siku kutoka BBC Idhaa ya Kiswahili https://www.youtube.com/channel/UCoerKKIKIMlDYaVFSTlsWGw