Skip to main content
Skip to main content

Gavana Barasa asema ujenzi wa hospitali ya rufaa ya Kakamega utakamilika ndani ya miezi mitano ijayo

  • | Citizen TV
    139 views
    Duration: 1:15
    Gavana wa kakamega Ferdinand Barasa ametangaza kwamba Hospitali ya mafunzo na rufaa ya kakamega itakuwa tayari kutumika ndani ya miezi mitano ijayo. Barasa alitoa taarifa hiyo wakati wa ziara ya ukaguzi wa kazi za ujenzi zinazoendelea katika hospitali hiyo, ambapo alitathmini maendeleo yaliyopatikana hadi sasa. Alionyesha kuridhika na kasi ya mradi huo.