- 224 viewsDuration: 1:25watoto zaidi ya 100 kutoka kaunti mbalimbali wamepata mwanga mpya wa matumaini baada ya kupokea vifaa vya kuwasaidia kusikia katika Hospitali ya Rufaa ya Kaunti ya Kapsabet. Hatua hiyo inalenga kuboresha maisha ya watoto wenye changamoto hiyo. Mpango huo wa hisani, uliowaleta pamoja wataalamu wa afya na wahisani, uliwalenga watoto kutoka familia zisizojiweza ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa katika masomo na mawasiliano ya kila siku kutokana na ulemavu wa kutosikia.