- 8,886 viewsDuration: 3:03Idadi ya waliofariki kwenye ajali za barabarani katika kipindi cha saa 72 imefikia watu 36 baada ya watu watano zaidi kufa kwenye ajali nyingine leo asubuhi. Aidha watu wawili walijeruhiwa kwenye ajali hiyo iliyotokea katika eneo la Kedowa katika barebara kuu ya Kericho kuelekea Nakuru. Na kama anavyoarifu Mary Muoki, ajali hiyo ilihusisha gari aina ya Toyota Probox na trela.