- 1,799 viewsDuration: 1:20Baraza la Wazee wa Kalenjin limewataka vijana nchini kukataa kutumiwa na wanasiasa kuzua vurugu, huku uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 ukikaribia. Wakizungumza mjini Eldoret, wazee hao wakiongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la wazee YA Kalenjin maarufu Myoot Council of Elders, Benjamin Kitur, wamewataka wanasiasa na wafuasi wao kudumisha amani na kuwaruhusu viongozi kuwasilisha sera zao kwa wananchi, kabla ya wapiga kura kufanya maamuzi yao kupitia kura mwaka 2027.