- 9,444 viewsDuration: 2:49Familia moja hapa jijini Nairobi inalilia haki baada ya binti yao mwenye miaka 14 kuchomwa vibaya kwa maji ya moto shuleni. Mwanafunzi huyo wa shule ya upili ya wasichana ya Mumbuni kaunti ya Machakos sasa amelazimika kukatiza masomo yake kwa mwezi wa pili sasa kutokana na majeraha hayo. Sasa familia yake inasema imewachwa kugharamia matibabu yake huku kamanda wa polisi Machakos Monica Kimani akisema polisi wanaendelea kuchunguza kisa hicho