- 208,494 viewsDuration: 3:50Kizaza kilishuhudiwa katika Forodha ya Pamoja ya Namanga baada ya Basi la Kampuni ya KIDIA ONE EXPRES kunaswa likisafirisha nyoka aina ya Chatu ambaye alikuwa akisafirshwa Jijini Nairobi kutoka Jiji la Dar es salaam nchini Tanzania akiwa ndani ya Sanduku. Maafisa wa Kukagua Mizigo mpakani waligundua Sanduku Lisilo la kawaida likiwa na maelezo ya mzigo wa Vipuri vya Magari lakini walipofungua sanduku hilo walipata chatu. Tayari Dereva wa Basi hilo pamoja na Utingo wake wanazuiliwa wakitarajiwa kufikisha mahakamani na kushtakiwa kwa kosa la Ulanguzi wa wanyamapori.