Kenya inaweza tu kuafikia ruwaza yake ya kuwa nchi iliyostawi kwa kutekeleza hatua kadhaa ikiwa ni pamoja na kutumia sayansi na teknolojia kupitia kwa ufadhili wa utafiti na ubunifu, kuhamisha teknolojia na kufanya biashara ya utafiti na ubunifu. Akiongea wakati wa mkutano wa wadau leo kabla kuanza kwa wiki ya Sayansi, teknolojia, utafiti na ubunifu, katibu wa sayansi, utafiti na ubunifu, Prof. Shaukat Abdulrazak, alikariri kwamba Kenya iko kwenye mwelekeo ufaao lakini ushirikiano zaidi unahitajika kutoka kwa wadau wa sekta hiyo.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive