- 8,535 viewsDuration: 2:45Naibu kinara wa Jubilee Dkt. Fred Matiang’i amemkosoa Rais William Ruto kwa matamshi yake dhidi ya Rais mstaafu Uhuru Kenyatta, ambaye amemtaja kama mfadhili wa upinzani. Matiang’i anasema matamshi ya Rais yanashusha hadhi ya afisi ya Rais. Akizungumza Nyamira katika hafla ya mazishi, Matiang’i amemtaka Rais Ruto kuwajibikia kazi aliyopewa na wananchi badala ya kutoa cheche za maneno kila mara.