- 144 viewsDuration: 1:29Wadau wa afya ya jamii walitambuliwa katika siku ya kitaifa ya uhamasishaji wa funza katika jukumu lao la kufanikisha vita dhidi ya mashambulizi ya funza nchini. Akizungumza katika hafla hiyo, mkurugenzi mtendaji wa Ahadi Kenya Trust daktari Stanley Kamau alishukuru msaada wa serikali huku wakilenga kuondoa visa vilivyosalia ili kuhakikisha hakuna waathiriwa wa funza nchini huku wakiwahimiza wakazi kuzingatia usafi zaidi.