- 318 viewsDuration: 1:53Wanaharakati mjini Mombasa wametaka tume ya uchaguzi na mipaka IEBC kufanya hamasiho zaidi ili kuongeza idadi ya wapiga kura wapya. Zoezi hilo likitazamiwa kukamilika hii leo, wametaka mikakati zaidi kuwekwa ikizingatiwa kuwa wakenya wengi bado hawajajiandikisha. Wakiongea mjini Mombasa wakati wa maadhimisho ya miaka 10 ya shirika la haki Africa wanaharakati hao pia wametangaza kuwa wakenya wengi wamepata ufahamu wa haki zao za kimsingi ikiwemo kushiriki katika uchaguzi.