Skip to main content
Skip to main content

Viongozi wa kiislamu katika Kaunti ya Nandi wamtaka mwenyekiti wa SUPKEM Hassan Ole ajiuzulu

  • | Citizen TV
    164 views
    Duration: 2:16
    Viongozi wa Kiislamu katika Kaunti ya Nandi wanamshinikiza mwenyekiti wa SUPKEM Hassan Ole naado ajiuzulu mara moja. Hii ni baada ya kunaswa kwenye kamera za CCTV akifyatua risasi kuelekea kwa waandamanaji waliokuwa wakipinga uongozi wake. Wakizungumza katika Msikiti wa Jamia, huko Kapsabet, viongozi hao walimtaka Ole naado aondoke ili uchunguzi kamili ufanywe kuhusu tukio. Aidha Viongozi hao pia wametoa wito kwa Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai kuchukua hatua haraka na kuanzisha uchunguzi.