Kauli za wito wa umoja zilisheheni katika Jukwaa la Sherehe za Mawakili wa Mashariki ya Chini, huku viongozi akiwemo Gavana wa Machakos, Wavinya Ndeti, na Kiongozi wa Wiper, Kalonzo Musyoka, wakisisitiza umuhimu wa viongozi kuungana ili kukabiliana na hali ngumu ya uchumi.
Gavana Ndeti pia alionyesha wasiwasi wake kuhusu ongezeko la kodi kwenye mishahara ya wafanyakazi na hali mbaya ya sekta ya afya nchini. Kwa upande wake Kalonzo alithibitisha kujitolea kwake kwa uadilifu na kupigana na rushwa.Viongozi hao waliwaomba Wakenya kukumbatia umoja na kutaka uongozi unaowajibika ambao unaweka maslahi ya wananchi mbele.