- 146 viewsDuration: 1:50Wadau wa elimu katika eneo la Nyatike kaunti ya Migori wametaka kuwepo kwa mkakati shirikishi ili kukabiliana na ongezeko la visa vya mimba za utotoni na kuenea kwa ugonjwa wa Ukimwi miongoni mwa vijana katika eneo hilo. Wakiongozwa na mbunge wa Nyatike Tom Odege, washikadau hao walisisitiza haja ya kuwahusisha vijana katika michezo na shughuli nyingine za kujenga mienendo bora katika jamii......Walibainisha kuwa utangamano huo utasaidia kukuza vipaji na kupunguza muda unaotumika kwenye tabia zinazowaweka vijana hatarini.....