Waziri wa ardhi, ujenzi, nyumba na ustawi miji Alice Wahome ameonya kuhusu hatua kali za kisheria dhidi ya mtu yeyote atakayepatikana na hatia ya kuhusika na kuanguka kwa jengo la ghorofa kadhaa katika eneo la South C jijini Nairobi na kusababisha kifo cha mtu mmoja.Wahome, ambaye leo alitembelea eneo hilo kwa mara ya kwanza, alisema msanifu majengo na wahandisi waliohusika wana hatari ya kupoteza leseni zao ikiwa uchunguzi utathibitisha jukumu la kihalifu kwa upande wao. Shughuli ya kumtafuta mtu wa pili aliyekwama katika jengo hilo inatarajiwa kukamilika Jumanne.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive