Serikali imeimarisha juhudi za kupunguza athari za kiangazi katika Maeneo Kame kwa kuharakisha ujenzi wa visima vya maji na kuimarisha utunzaji wa chemichemi muhimu za maji. Katibu wa unyunyiziaji mashamba maji, Ephatus Kimotho, amesema kuwa idara hiyo tayari imechimba visima kadhaa vya maji katika maeneo yanayokumbwa na ukame, yakiwemo Kaunti ya Kajiado ambayo kwa sasa inakabiliwa na makali ya kiangazi. Mpango huu unalenga kuboresha upatikanaji wa maji kwa jamii na mifugo wakati wa vipindi virefu vya ukame.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive