- 12 viewsGavana wa Kiambu Kimani wa Matangi jioni hii anadai vita vya kisiasa baada ya biashara zake kubomolewa na maafisa wa shirika la reli kwenye zoezi la ubomoaji lililofanywa jana usiku. Kwenye oparesheni hiyo, Maduka yaliyo kwenye ardhi ya shirika la reli karibu na uwanja wa Nyayo, Nairobi yalibomolewa, Huku shirika la reli likisema kuwa lilitoa ilani kwa biashara hizo kuondolewa kutoa upanuzi wa njia kwa matayarisho ya mashindano ya AFCON. Lakini Gavana wa Matangi anasema hawakupata ilani.