- 28 viewsHuduma za afya katika hospitali za umma hapa jijini Nairobi zimeendelea kutatizwa kwa siku ya tatu hii leo, wahudumu wa afya wakidai mishahara ya kati ya mwezi mmoja na mitatu. Madaktari na maafisa kliniki wamekuwa wakisusia kazi wakitaka kulipwa na serikali ya kaunti ya Nairobi. Sasa wanamlaumu gavana Johnson Sakaja kwa kufumbia macho swala hili, wauguzi nao wakitarajiwa kujiunga na mgomo kuanzia hapo kesho