- 309 viewsDuration: 1:40Moto wa mara kwa mara katika mbuga ya kitaifa ya tsavo na hifadhi za kijamii kaunti ya Taita Taveta imesababisha wanamazingira na maafisa wa serikali za kaunti kutoa wito kwa jamii kushirikiana ili kukabiliana na visa hivyo. Aidha serikali ya kaunti imetengeneza sera maalum ya kukabiliana na moto. Wakizungumza mjini Voi washikadau mbalimbali wa kukabiliana na moto wakiwemo maafisa wa shirika la kulinda na kuhifadhi wanyamapori KWS na wale wa misitu wanalenga kutengeneza sera ambaYo wadau wote watashirikiana kukabili suala hilo.