- 256 viewsDuration: 2:02Wamiliki ardhi Pamoja na wakazi 2,000 wanaoishi katika hifadhi ya Wanyama pori eneo la Pardamat eneo bunge la Narok Magharibi wamepongezwa kwa kukubali shughuli ya kuondoa ua wa kilomita 400 ili kutoa nafasi kwa Wanyama pori. Wakizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa filamu ya mazingira katika shule ya mafunzo ya Mbuga na Utalii ya Maasai Mara, washikadau wamepongeza hatua hiyo wakiitaja kama kuu itakayositisha uhasama baina ya Wanyama pori na binadamu mbali na kuimarisha utalii.