- 290 viewsDuration: 1:35Idara ya polisi katika eneo bunge la Butula imenasa lita 290 za pombe haramu ya chang'a inayokadiriwa kuwa ya thamani ya shilingi elfu mia tatu ikiwa imefichwa katika nyumba moja mjini bumala. Kamanda wa polisi katika eneo bunge hilo Eunia Onyancha amesema kuwa operesheni ya kusaka pombe hiyo imetokana na taarifa walizopokea kutoka kwa wananchi na inakisiwa kuwa pombe hiyo ilikua imefichwa hapo ikisubiri kusafirishwa maeneo mengine.