Tume huru ya uchaguzi na uratibu wa mipaka hapa nchini-IEBC imemteua mmoja wa wafanyikazi wake kuwa kaimu msimamizi wa shughuli zake.. IEBC imemteua Moses Ledama Sunkuli kwa wadhifa wa kaimu afisa mkuu mtendaji kwa kipindi cha miezi sita. Uteuzi wa Sunkuli unafuatia kujiuzulu kwa Marjan Hussein siku mbili zilizopita, na kuacha pengo la usimamizi. Sunkuli ambaye ni afisa aliyehudumu katika tume hiyo kwa muda mrefu, anatarajiwa kusimamia shughuli za kila siku za tume hiyo, kutekeleza maamuzi ya tume na kusaidia katika utekelezaji wa mageuzi yanayoendelea wakati wa kipindi hicho cha mpito.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive