Gavana wa Nyandarua Dkt. Moses Kiarie Badilisha, mwanasheria mkuu wa kaunti hiyo, maafisa wa ununuzi pamoja na maafisa wengine wanaoshughulikia fedha katika kaunti hiyo, wameagizwa kurejesha fedha baada ya kamati ya seneti kuhusu usimamizi wa fedha za umma kugundua kwamba usimamizi wa kaunti hiyo ulikiuka sheria, hatua iliyosababisha wakazi wa kaunti hiyo kupoteza mabilioni ya fedha. Hii ni baada ya serikali ya kaunti hiyo kusitisha kandarasi ya shilingi bilioni 1.5 baada ya kutumia shilingi Milioni 900 kuondolea mbali madini ya asbetos kutoka kwenye mapaa ya hospitali ya matibabu maalum ya JM Kariuki. Abdiaziz Hashim ana taarifa kamili.
Connect with KBC Online;
Subscribe to our channel: https://t.ly/86BKNc
Follow us on Twitter: https://twitter.om/KBCChannel1
Find us on Facebook: https://www.facebook.com/kbcchannel1TV
Check our website: https://www.kbc.co.ke/
#kbcchannel1 #news #kbclive