- 52 viewsNi afueni kwa wakazi wa eneo la Barambate, huko North Horr kaunti ya Marsabit, kufuatia juhudi za mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, kuwachimbia visima vya maji na kuwatengezea mifereji. Hali hii ikitarajiwa kuwaondolea dhiki ya kutafuta maji, huku makali ya kiangazi yanapozidi kuwatatiza wafugaji wa maeneo hayo.