- 225 viewsDuration: 2:26Viongozi wa makanisa sasa wanawataka wanasiasa kutuliza kelele za siasa na badala yake kuwahudumia wakenya. Askofu mkuu wa kanisa la Kianglikana nchini Jackson Ole Sapit, akisema nyuzi joto za sasa zinazidi kupanda, zaidi ya mwaka mmoja unusu kabla ya uchaguzi mkuu. Naye Askofu Mkuu wa kanisa katoliki jimbo la Nyeri Anthony Muheria, akionya dhidi ya swala la ukame nchini kuingizwa siasa akisema kuna hatari kubwa.